Dalili Za Upungufu Wa Nguvu Za Kiume

Dalili Za Upungufu Wa Nguvu Za Kiume

Dalili Za Upungufu Wa Nguvu Za Kiume-In this article you will learn Male impotence is a condition of not being able to make love fully or not being able to stop it properly, sexual activity involves the mind, hormones, nerves, emotions and blood vessels, muscles. Studies show that in five (5) men then one of them he has an impotence problem.

Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kuto kuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalo hitaji tiba.

Tatizo hili huwanyima sana watu raha na kupelekea kuwa na mawazo, migogoro katika mahusiano.Watu wenye changamoto hii mara zote wanahitaji dawa zisizo na madhara(virutubisho lishe) vilivyotokana na mimea na matunda na kubadilisha mitindo yao ya kimaisha(Lifestyle changes) ili kuweza kurudisha hali zao na kuondoa tatizo.

Dalili Za Upungufu Wa Nguvu Za Kiume:

Zifuatazo ni baadhi ya dalili za upungufu  wa nguvu za kiume;

1) Kukosa Hamu Ya Kufanya  Tendo La Ndoa.

Tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa mwanaume ni moja wapo ya dalili za upungufu wa nguvu za kiume na linaweza kusababishwa na sababu nyingi sana.Sababu hizo zinaweza kuwa za kimaumbile au kisaikolojia au za mchanganyiko wa sababu za kimaumbile na sababu za kisaikolojia.Baadhi ya sababu za tatizo hili ni pamoja na;

a) Msongo Wa Mawazo (Depression).

Msongo wa mawazo ni ugonjwa wa kisaikolojia unaohusisha hali ya kuwa na mawazo makali kwa muda mrefu yanapolekea kukosa raha kutokana na kujihisi si mtu wa thamani au kukosa starehe katika vitu ulivyozoea kuvifanya na kukufurahisha hapo awali.Mawazo ya namna hii huathiri mwenendo wako wa maisha yako ikiwa ni pamoja na kukosa matamanio ya kimapenzi.

b) Matumizi Ya Madawa Na Pombe.

Matumizi ya baadhi ya madawa na  unywaji wa pombe wa kupindukia vinaweza kupelekea tatizo hili la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa.Madawa yanayochangia tatizo hili ni pamoja na;Madawa ya presha ya kupanda(Anti hypertensive drugs), madawa ya kuondoa msongo wa mawazo, madawa yote yanayozuia ufanyaji kazi au uzalishaji wa testosterone, kwa mfano, cimetidine,finasteride na cyproterone n.k

c) Mawazo Mengi Na Uchovu.

Matatizo ya kikazi na hadhi yako kazini vinaweza kuchangia kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa.Kama unabezwa sana kazini na kujiona hutimizi kazi yako ipasavyo au kama unachoka sana kazini pia  vinaweza kupelekea kukosa hamu ya kufanya mapenzi pindi urudipo nyumbani kwani mahusiano ya kimapenzi yanahitaji yatengewe muda wa kutosha.

d) Kuwa Na Umri Mkubwa.

Kiwango cha homoni ya testosterone inayohusika na hisia za kimapenzi kwa mwanaume hupungua kwa asilimia 1-2 kila mwaka kadri mwanaume anavyozidi kuwa na umri mkubwa.Kiwango cha testosterone kikishuka katika mwili wa mwanaume humfanya asiwe na nguvu, ashindwe kutuliza mawazo kwenye jambo alifanyalo na apoteze hamu ya kufanya mapenzi.

e) Mahusiano Yaliyopo Baina Ya Mwanaume Na Mwanamke.

Matatizo ya kimahusiano kati ya mwanaume na mwanamke yana mchango mkubwa sana katika kusababisha tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa, mfano uwepo wa migogoro kati ya mume na mke, ukosefu wa amani na furaha katika  mahusiano huchangia sana mwanaume kukosa hamu ya kufanya mapenzi.

Kama mahusiano yako na mpenzi wako yamekuwa ya miaka mingi sana, unaweza kuwa umemzoea mno mkeo kiasi kwamba ukaanza kukosa hamu ya kufanya naye tendo la ndoa.Hili nalo hutokea mara nyingi.

f) Matatizo Ya Kiafya.

Matatizo ya kiafya ya muda mrefu(chronic diseases) husababisha kupungua kwa hamu ya kufanya tendo la ndoa, mfano tatizo la kisukari, tatizo la presha, tatizo la moyo, tatizo la kansa ya muda mrefu, na hali ya kuwa na unene uliozidi kiwango(obesity) n.k

2) Kutokuwa Na Uwezo Wa Kurudia Tendo La Ndoa Zaidi Ya Mara Moja.

Mwanaume mwenye changamoto ya upungufu wa nguvu za kiume akishakamilisha mshindo mmoja wa tendo la ndoa basi anakua hana uwezo tena wa kurudia mshindo mwingine.Hali hii husababishwa na kutokuwepo na mshukumo wa damu wa kutosha kwenye mishipa ya uume.

3) Kutokuwa  Na Uwezo Wa Kusimamisha Uume Kabisa.

Kwa kawaida uume wa mwanaume aliyekamilika(rijali) unaposimama, hutakiwa kuwa imara kama msumari, lakini kwa mwanaume mwenye changamoto ya upungufu za nguvu za kiume uume wake hata ukisimama hubakia kuwa lege lege na unaweza kusinyaa wakati wowote.

Tatizo hili ni matokeo ya kulegea kwa mishipa ya uume ambayo ndio huufanya uume usimame barabara.

4) Kuwahi Kufika Kileleni.

Kuwahi kufika kileleni ni hali ambayo inampata mwanaume mwenye changamoto ya upungufu wa nguvu za kiume ambapo hutoa shahawa kabla ya kuanza tendo la ndoa au muda mfupi tu baada ya kuanza tendo la ndoa, bila yeye mwenyewe kukusudia.Kwa kawaida mtu mwenye tatizo la kuwahi kufika kileleni hutoa mbegu zake za kiume hata baada ya maandalizi kidogo sana.

5) Kuchoka Sana Baada Ya Tendo La Ndoa Na Hata Kukinai Kabisa

Hii ni moja wapo ya dalili za upungufu wa nguvu za kiume.Hali hii huwapata wanaume wenye changamoto ya upungufu wa nguvu za kiume ambayo wakati mwingine huambatana na usingizi mzito(Kulala fofofo).

6)  Kuhisi Maumivu Wakati Wa Tendo La Ndoa/Baada Ya Tendo La Ndoa.

Hii pia ni moja wapo ya dalili za upungufu wa nguvu za kiume, hali hii huweza kuchangiwa na kauthirika kwa tishu za uume ambazo hutokana na upigaji wa punyeto kupita kiasi.

7) Kuchelewa  Sana Kufika Kileleni/Kushindwa Kufika Kileleni Kabisa.

Ni ile hali ya mwanaume kuchukua muda mrefu kutoa manii wakati wa kushiriki tendo la ndoa.

Kwa kawaida mwanaume anatakiwa afike kileleni/kutoa manii kwa muda usiozidi dakika 30 wakati wa kushiriki tendo la ndoa.Kwa hiyo mwanaume anaposhiriki tendo la ndoa na kuchukua muda mrefu bila kufika kileleni anahitaji uchunguzi ili kubaini chanzo cha tatizo.

Sababu Za Upungufu Wa Nguvu Za Kiume:

Zifuatazo ni baadhi ya sababu za tatizo la upungufu wa nguvu za kiume;

  1. Uzito kupita kiasi na unene uliozidi.
  1. Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi.
  1. Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe.
  1. Kuwa na mawazo na wasi wasi.
  1. Kuwa na tatizo la kibofu cha mkojo.
  1. Matumizi makubwa ya dawa zenye kemikali za kutibu magonjwa kama kansa, vidonda vya tumbo, kisukari, presha, magonjwa ya moyo nk.
  2. Tabia za kujichua kwa muda mrefu.
  1. Umri hasa wazee.

What’s your take on this? We believe this article was helpful, if yes, don’t hesitate to share this information with your friends on Facebook, Twitter, WhatsApp, and other Social Platforms Thanks so much for sharing.

Leave your thoughts